Skip to main content

VIJANA KAJIADO KASKAZINI KUPATA AJIRA







Baada ya lalama ya ajira kwa vijana hasa kutoka kwa wakaazi wa Kajiado Kaskazini, zaidi ya vijana 100,000 kutoka kwa vitongi na vijiji hapa jimboni watapata mafunzo na kisha baadaye kujipatia ajira  katika maswala ya kuweka mazingira safi na kushinikiza matendo ya afya bora.

Ni swala ambalo limeungwa mkono na wazazi pamoja na wadau ambao walikuwa wamekata tamaa na swala la ajira kwa vijana wao hasa Kajiado Kaskazini. 

Hali hii imejiri baada ya Mbunge wa Kajiado Kaskazini Mheshimiwa Joseph Manje kurai Bunge la Kitaifa kupitia mswaada uliyotolewa  kuwa ipo haja ya serikali kubuni ajira mbalimbali hasa kwa rika la vijana ambao wamesoma lakini hawana ajira rasmi na isiyorasmi.

Mbunge wa Kajiado Kaskazini Kaskazini Manje anasema kuwa hakuna kijana katika jimbo lake atawachwa nje pindi nafasi za ajira kwa vijana zinapojitokeza. 

Comments

Unknown said…
Thanks alot for remembering the youths
Unknown said…
I would like to join