Skip to main content

Posts

Showing posts with the label KIMATAIFA
Waziri Balala akizungumza na wadau katika sekta ya utalii  nchini. Kenya imetenga shilingi milioni 500 katika kusaidia kwenye sekta ya utalii hii nikufuatia hofu ya mlipuko wa COVID 19 maarufu kama Virusi vya Corona . Akizungumza na waandishi wa habari waziri wa utalii anasema hela hizo zitatumika  kurejesha imani kwa wadau hasa watalii wa kila mara humu nchini. Kadhalika waziri Balala anasema kuwa hela zingine zitatumika katika kupanga mkakati wa kuhakikisha  kero ya virusi vya Korona havisambai kote nchini. "Serikali imetenga shilingi milioni 500 kutoka mfuko wa hazina ya kitaifa  ilikuhakikisha kuwa  janga la ukosefu wa utalii na kusambaa kwa virusi vya Korona vina kabiliwa vilivyo ."asema waziri Balala.

KASHFAA YA PESA NHIF

MKURUGENZI WA BIMA YA TAIFA NHIF GEOFREY GITAU Viongozi 14 kutoka bima ya taifa NHIF watafikishwa  mahakamani  mapema jumanne ilik kujua hatma yao kuhusu kesi inayowakabili inayayohusu ubadhilifu wa fedha na kosa la kutoshirikiana na maafisa jasusi  kuhusu matumizi ya fedha hizo za umma  Mkurugenzi wa mashtaka ya umma Nordin Hajji  katika taarifa kwa  vyombo vya habari alisema  wawili hao Geofrey Gitau ambaye ni mkurugenzi wa  bima ya taifa pamoja na mwenzake  anayesimamia maswala ya fedha na uwekezaji  Wilbert Kiplagat  wanakesi ya kujibu hivyo kulazimika kulala rumande kwa siku ya pili mtawalia ‘’Maafisa walikataa kuwasilisha stakabadhi zinazo orodhesha namna walivyo walipa kampuni ya webtribe mamillioni ya hela.’’anasema hajji.