Skip to main content

Posts

Showing posts from May, 2020

SENETA MARY:NINA IMANI NA UHURU

Seneta mteule wa kaunti ya Kajiado Mary Seneta ameapa kuwa yeye ni mwaminifu kwa Mwenyekiti wa chama cha Jubilee rais Uhuru Kenyatta huku akiongeza kuwa hakuwa na maana fishe licha siasa zinaendelea katika chama hiyo.  Akizungumza mbele ya jopo la nidhamu katika chama cha Jubilee inayoongozwa na kinara mkuu wa seneti Irungu Kangata, Seneta Mary anasema kuwa kutokana na utendaji kazi wake katika chama cha TNA hadi sasa wa chama tawala Jubilee kuwa hajawai kiuka  ilani ya chama na utendaji kazi wa chama. Aidha Makataa ya siku 14 imetolewa  kwa maseneta hao ambao wamechukuliwa hatua za kinidhamu ya kutohudhuria mkutano wa chama pale ikulu, hatua ambayo itaeleza hatma ya maseneta hao. Naye kwa upande wake katibu katika chama cha Jubilee Raphael Tuju alisema ipo haja ya heshima kudumu katika chama na wakiukaji kuheshimu muhimili wa uongozi wa taifa. 

500 WAFAIDIKA NA CHAKULA CHA MANJE

Kufuatia tamko la rais Uhuru Kenyatta kuwa mipaka ya Kenya na Nchini jirani kufungwa kwa siku 30 zaidi.Wakaazi wa eneo la Gishagi  katika Jimbo la Kajiado Kaskazini wamepata msaada wa chakula kutoka mbunge wao Mh. Joseph Manje kupitia Wakf wa Manje maarufu kama Manje Foundation. Ajuza na vijana 500 wamefaidika na msaada hiyo ambayo  imewafaidi pakubwa tangu kuzuka kwa janga la Korona. Msaada huo ambayo ni kupitia muungano na Saytha Sai  Ikishirikiana na Wakf wa Manje umesema kuwa zoezi hili litakuwa endelevu na jamii maskini zitazidi kufaidika kupitia kwa msaada  mbalimbali ikiwemo, barakoa na viyeyuzi. Akizungumza mmoja wa wakaazi hao alinena kuwa Mheshimiwa Manje amekuwa akiwa kumbuka maajuza hao na kundi la vijana kila mara kando na mlipuko wa Janga la Korona inchini. 

VIJANA KAJIADO KASKAZINI KUPATA AJIRA

MBUNGE MANJE ADHIBITI CORONA

Maeneo 23 madogo katika jimbo la Kajiado Kaskazini yamenufaika na vituo vya kunawa mikono, pamoja na barakoa zaidi ya 5,000 zilizotolewa katika mfuko wa Hazina ya majimbo maarufu kama NGCDF chini ya usimamizi mkuu wa Mbunge wa Kajiado Kaskazini Mheshimiwa Joseph Manje. Hafla hii ilizinduliwa na Mwenyekiti wa hazina hii mapema hapo jana na kuhakisha kuwa zoezi hili linakuwa endelevu kwa umma.  Kando na taasisi mbalimbali kupendekeza kuwa mbunge wa Kajiado Kaskazini ni miongoni mwa mfuno mwema wa kuigwa kutokana na uchapakazi kazi, baadhi ya majimbo nchini wameomba kupitia muhimili wa bunge kuandaa safari maalum ya kuzuru miradi ambayo mbunge Manje ameanzisha hadi kufikia sasa.  Kadhalika Manje anaema ipo haja ya kusimama kidete na kuhakikisha kuwa Kajiado Kaskazini inapambana na janga la Korona,  kwa sasa visa viwili vilivyo ripotiwa kuwa ni Codiv +  vimebainika kuwa siyo hii ni kwa mujibu wa wizara ya afya kupitia kwa mganga mkuu. 

WE THE COSMOPOLITAN SHARE ON THE BBI

kajiado press