Skip to main content

Posts

Showing posts from June, 2020

TUSIWASAHAU WATOTO WA MTAANI:MBUNGE MANJE

kajiado press

TUSIWASAHAU WATOTO WA MTAANI:MBUNGE MANJE

kajiado press

MANJE AISHANGAZA DUNIA

kajiado press

Miradi Inahitaji umakinifu ;Mbunge Manje kwa wahandisi

kajiado press

MBUNGE MANJE ASEMA LUGHA KAJIADO KASKAZINI NI MAENDELEO

kajiado press

Mbunge Manje ajitosa ulingoni kuwatumikia wananchi

kajiado press

CHONDE CHONDE WAHALIFU:KAMANDA RASHID ASEMA

Kamanda wa polisi Kajiado Kaskazini Rashid Mohammed ameapa kuimarisha usalama Katika eneo hilo ambalo makundi hasi ya ujambazi yameanza kuchipuka. Akimhakikishia Mbunge wa Kajiado Kaskazini Mheshimiwa Joseph Manje kamanda Mohamed amesema kuwa kupitia maafisa wapya ambao  wanasimamia kituo cha Ongata Rongai na Ngong visa hivyo vitapungua pakubwa. Kwa upande wake mbunge Manje ameirai idara hiyo ya usalama kuwa macho na kuhakikisha raia wako salama na pia mahusiano baina ya idara ya polisi na umma inakuwa sawa iliupashwaji wa taarifa  za kiintelijensia ni wa kuaminika na kwa muda unaofaa.

MANJE ALIPA ADA

Ni afueni kwa wazazi na wanao Kajiado Kaskazini baada ya mbunge Manje kulipa ada kupitia mfuko wa hazina wa CDF maarufu kama basari. Mbunge Manje alizuru baadhi ya mashule ambako wanafunzi tajika waliopitia mchujo katika kamati mbalimbali jimboni wameweza kulipiwa ada.  Aidha huku umma hasa wa Kajiado Kaskazini ukizidi kusubiria tamko kutoka kwa wizara ya elimu kuhusu tarehe rasmi ya kufungua mashule, imemlazimu Mbunge Manje ambaye rekodi yake katika elimu ikizidi kung'aa kujitwika mzigo na kuhakikisha hamna mwanafunzi atakaye salia nyumbani. Ziara hiyo ya kushtukiza imewaacha baadhi ya wazazi wakiwa na furaha hii ni kutokana na utendaji kazi wa mheshimiwa  Manje.  Ali Omar mmoja wa  mzazi katika eneo la Oloolua amepongeza mheshimiwa na kurai kuwa hakuna kiongozi atakaye mbandua Mheshimiwa katika kiti kufuatia maendeleo ambayo yanazidi kupatikana Kajiado Kaskazini kilakuchao. 

KOSA BARAKOA TIWA MBARONI

Naibu Kamishna Kajiado Kaskazini Bwana Tom Anjere atoa agizo la kuwasukuma ndani wadau wanaokaidi masharti ya kujikinga na janga la COVID-19. Taarifa hii ni kufuatia shinikizo kutoka kwa idara za usalama katika serikali kuu zikirai kuwa janga la Korona ingali inaangamiza watu na maambukizi kuzidi kila kuchao.  Aidha Kaunti ya Kajiado ni miongoni mwa kaunti zilizo andikisha idadi chache ila idara husika imebaini kuwa maeneo ya miji katika kaunti hii yameanza mapuuza na kudhania kuwa hali imerejea kawaidi.  Duru zakuaminika zinasema kuwa endapo raia mwema atapatikana hajavalia barakoa atatiwa mbaroni na kushatakiwa kwa kosa la kuwaweka wakenya hatarani na maambukizi ya KOVIDI 19.  Kwa sasa zoezi limeng'oa nanga nawatuhumiwa watafikishwa  Kortini mnamo siku ya jumatatu na Alhamisi mtawalia.