Skip to main content

Posts

Showing posts from June, 2020

MANJE ALIPA ADA

Ni afueni kwa wazazi na wanao Kajiado Kaskazini baada ya mbunge Manje kulipa ada kupitia mfuko wa hazina wa CDF maarufu kama basari. Mbunge Manje alizuru baadhi ya mashule ambako wanafunzi tajika waliopitia mchujo katika kamati mbalimbali jimboni wameweza kulipiwa ada.  Aidha huku umma hasa wa Kajiado Kaskazini ukizidi kusubiria tamko kutoka kwa wizara ya elimu kuhusu tarehe rasmi ya kufungua mashule, imemlazimu Mbunge Manje ambaye rekodi yake katika elimu ikizidi kung'aa kujitwika mzigo na kuhakikisha hamna mwanafunzi atakaye salia nyumbani. Ziara hiyo ya kushtukiza imewaacha baadhi ya wazazi wakiwa na furaha hii ni kutokana na utendaji kazi wa mheshimiwa  Manje.  Ali Omar mmoja wa  mzazi katika eneo la Oloolua amepongeza mheshimiwa na kurai kuwa hakuna kiongozi atakaye mbandua Mheshimiwa katika kiti kufuatia maendeleo ambayo yanazidi kupatikana Kajiado Kaskazini kilakuchao. 

KOSA BARAKOA TIWA MBARONI

Naibu Kamishna Kajiado Kaskazini Bwana Tom Anjere atoa agizo la kuwasukuma ndani wadau wanaokaidi masharti ya kujikinga na janga la COVID-19. Taarifa hii ni kufuatia shinikizo kutoka kwa idara za usalama katika serikali kuu zikirai kuwa janga la Korona ingali inaangamiza watu na maambukizi kuzidi kila kuchao.  Aidha Kaunti ya Kajiado ni miongoni mwa kaunti zilizo andikisha idadi chache ila idara husika imebaini kuwa maeneo ya miji katika kaunti hii yameanza mapuuza na kudhania kuwa hali imerejea kawaidi.  Duru zakuaminika zinasema kuwa endapo raia mwema atapatikana hajavalia barakoa atatiwa mbaroni na kushatakiwa kwa kosa la kuwaweka wakenya hatarani na maambukizi ya KOVIDI 19.  Kwa sasa zoezi limeng'oa nanga nawatuhumiwa watafikishwa  Kortini mnamo siku ya jumatatu na Alhamisi mtawalia.